INSIDE INAPATIKANA MADUKANI

FILAMU YA JADA ITAKUWA SOKONI 19.02.2015

JADA IPO SOKONI

JADA IPO SOKONI

Thursday, August 30, 2012

IMEVUJA SNURA AMWAGA UGALI, WEMA AMWAGA MBOGA


 KUKIWA hakujapoa vizuri baada ya ushoga wao kuvunjika, mwigizaji wa sinema Bongo, Snura Mushi hivi karibuni alifanya mahojiano katika Runing a ya EATV, Kipindi cha Hot Mix ambapo alianza dalili za kumvua Miss Tanzania 2006 na staa wa sinema za Bongo, Wema Sepetu ambaye aliwahi kuwa shosti wake mkubwa.
Kwa mujibu wa macho ya mashuhuda, Snura alisisitiza kuwa, ana siri nzito za Wema na siku akiamua kuzianika, basi mrembo huyo hatakatiza mitaani kwa aibu.
Kwa maneno ya Snura, kila aliyetazama kipindi kile alisema hata kama mcheza filamu huyo hakuzitaja moja kwa moja siri za mwenzake, lakini kila mtu anajua Wema anatembea na aibu yake.
“Sasa kama Snura hakutaka kuzitaja hizo siri, kusema vile tu si tayari ameshamuumbua mwenzake, kila mtu anajua Wema ana mambo mabaya,” alisema Nice, mdada anayemiliki saluni moja iliyopo Kijitonyama, Dar.
Kama hiyo haitoshi, tayari Snura yupo kwenye mchakato wa kuandaa filamu inayoitwa Uozo wa Super Star ambayo ndani yake ni Wema mwanzo mwisho. Filamu hiyo inaandaliwa na Kampuni ya Chuz Entertainment ya Tuesday Kihangala ‘Chuz’.
Habari nyingine zinadai kuwa mara baada ya kumwagana na Wema, Snura kwa sasa amejipeleka kwa Chuz ambako ameigiza baadhi ya ‘sini’ kwenye Tamthiliya ya Jumba la Dhahabu ambayo inaingia mtaani hivi karibuni.
WEMA AMTAHADHARISHA SNURA
Wakati Snura akiwa na mengi ya moyoni, kwa upande wake, Wema alitoa msemo wa Wahenga akimwambia Snura, Kimya Kingi Kina Mshindo.
Alimtaka Snura anyamaze na afute nia yake kwani yeye akianza kuzungumza ya kwake anaamini Snura hataweza hata kutembea mitaani.
“Nayasikia mengi sana anayozungumza Snura lakini mi ni muungwana, asinione nipo kimya. Nikiamua kufunguka sitaweza kusikia la mnadi swala wala la muadhini.
“Hakuna mtu asiyejua kama mimi ndiye nilikuwa naendesha maisha yake kama mke wangu. Kila nguo nzuri anayoivaa kwa sasa au pochi anayobeba ni fedha zangu. Namuomba kabisa asinichokonoe,” alisema Wema.
Akaongeza: Nimeshamlipia kodi ya nyumba Snura, nimeshamsaidia kulipa ada ya mtoto wake, sasa ni kwa nini asiniheshimu?”

Wednesday, August 29, 2012

JENNIFER KYAKA [ODAMA] KUACHIA FILAMU MPYA - CHOCOLATE

Kampuni ya J-Film 4 Life chini ya Mkurugenzi Jennifer Kyaka (Odama) inapenda kukujuza kuwa mwezi Septemba 2012 itaachia filamu mpya ya Chocolate.



Mdau wangu naomba ukifika huo mwezi, wahi dukani na kununua filamu hii ambayo itakufanya uwe mtu wa tofauti kwa yale yaliyoigizwa. Tumekuelimisha, tumekufundisha, tumeadibisha na kukuburudisha.

J-Film 4 Life imehakikisha filamu ipo katika viwango vya kimataifa hasa sauti na video kwa ujumla.

Pata kuona hii trailer

GARI LA KUKODI LAMTOKEA PUANI JACK CHUZ


 

                     Jacqueline Pentzel ‘Jack Chuz’. Na Richard Bukos
MWIGIZAJI wa Kibongo, Jacqueline Pentzel ‘Jack Chuz’, amejikuta kwenye wakati mgumu baada ya kukodi gari aina ya Toyota Spacio lenye namba za usajili T 750 BPK na kushindwa kulipa.
Bongowood iliambiwa na aliyemkodishia kuwa Jack Chuz alipewa gari hilo alitumie kwa siku tano kwa makubaliano ya kulipa elfu 50 kwa siku lakini zilipomalizika, alilirudisha na nusu ya fedha hivyo anasakwa na polisi kwa jalada la kesi namba RB/CH/ 6031/2012 huku bidada akijitetea kuwa alikuwa amesafiri.

BLOGU YA VITUKO VYA MTAA YAFUNGUKA KUMZUNGUMZIA ODAMA

Source: http://vitukovyamtaa.blogspot.com/2012/08/mfahamu-jennifer-kyakaodama.html

MFAHAMU JENNIFER KYAKA(ODAMA)

 
Jina Kamili: Jennifer Kyaka
A.k.a: Odama
Fani : Uigizaji
Kuzaliwa: 1983
Alikozaliwa: Bugando, Mwanza
Umri: 29
Makazi: Kinondoni - Biafra, Dar
Ndoa: Hajaolewa
STAA hot cake katika tasnia ya filamu za Kibongo, Jennifer Kyaka ‘Odama’ ametokelezea kunako Hot 2 Hot na kuweka plain kuwa katika mafanikio aliyoyapata hakuna mkono wa mwanaume kama ilivyo kwa wasichana wengine mastaa wa mjini.
Odama alitiririka kuwa amekuwa akifanya kazi kwa bidii na kile anachokipata ndicho anachofanyia mambo yote ya maendeleo ambapo hadi unaposoma hapa, anamiliki kampuni yake ya filamu ya J-Film For Life, magari mawili na mjengo.
“Mafanikio yangu yametokana na kazi zangu mwenyewe na hakuna mkono wa mwanaume, sitaki iwe hivyo ‘coz’ ndiyo maisha niliyoyachagua ya kutomtegemea mtu kwani kile ninachokipata kwenye filamu zangu ndicho kinachonipa maendeleo haya,” alisema Odama.
Hata hivyo, mwanadashosti huyo alisema kwa sasa ana mchumba na anatarajia kufunga ndoa mwakani.

BABY MADAHA NA ISABELA WANASWA TENA

MATUKIO ‘hot’ ya wasanii wawili Bongo, mwigizaji ambaye pia ni mwana-Bongo Fleva, Baby Joseph Madaha na chipukizi wa filamu, Isabela Francis ‘Vai wa Ukweli’ yamedhihirisha wao ni sikio la kufa,
Hivi karibuni, Baby Madaha alinaswa na kamera yetu kwa mara nyingine tena akiwa hajitambui kwa kulewa chakari kwenye Baa ya Uhuru Peak, Kinondoni jijini Dar ikiwa ni mara ya ishirini kwa kipindi kifupi kukutwa katika hali hiyo.
Baby Madaha alipoulizwa kwa nini anapiga ulabu hadi anazima tena mbele ya meneja wake, Mercey Kayuni, alidai ni maisha yake binafsi hivyo aachwe na maisha yake.
Wakati Baby Madaha akishauriwa kuacha ulevi kwani utampeleka pabaya, katika misele ya Ijumaa Wikienda akanaswa Isabela kwenye Ukumbi wa Dar West, Tabata jijini Dar kwa mara nyingine akifanya uchafu hadharani, yaani mambo ya chumbani akiwa na mwanaume aliyetajwa kwa jina moja la Bonny.
Isabela alipobanwa kuhusu kujilegeza kwa midume hakuwa na la kusema zaidi ya kuonekana kutojielewa.

AUNT LULU AIKIMBIA BONGO KUKWEPA MANENO



Lulu Mathias Semagongo ‘Aunt Lulu’.
KATIKA hali ya kushangaza, Mtangazaji maarufu Bongo, Lulu Mathias Semagongo ‘Aunt Lulu’ amefunguka kuwa atatimka nchini kwenda kuishi kusikojulikana.

Akizungumza na mwandishi  wetu  jijini Dar, Aunt Lulu alifunguka kuwa ameamua kukimbia mji kwani amechoshwa na manenomaneno ya walimwengu jijini.


“Nimechoshwa kwa kweli na kwa kuwa mipango yangu ya kuchomoka imetimia, acha nitimke Bango angalau nikapumzike kidogo nje ya hapa,”
alisema Aunt Lulu pasipo kutaja anakotimkia.

GENEVIEVE ARINGISHIA PETE YA UCHUMBA; KUFUNGA NDOA HIVI KARIBUNI?



Muigizaji wa kike mwenye mafanikio na anayetafutwa zaidi na watayarishaji wa filamu nchini Nigeria, Genevieve Nnaji huenda hivi karibuni akavaa shela ya harusi na kusema ‘I DO’.
Ripoti kutoka nchini Nigeria, zimesema kuwa muigizaji huyo na mama wa mtoto mmoja ameshachumbiwa na amekuwa akijionesha kwa watu kuwa muda si mrefu atakuwa mke wa mtu.
Kwenye akaunti yake ya twitter hivi karibuni aliweka picha inayomwonesha akiwa na pete ya uchumba na kuandika maneno yasemayo “kisses especially for U”
Kutokana na picha hiyo, mitandao mingi ya Nigeria imehitimisha kwa kusema kuwa tayari amechumbiwa.
Baadaye Genevieve aliandika kufafanua kuhusu picha hiyo iliyopo kwenye mtandao wa Instagram akisema, “I wear that ring on my right so people won’t think anything of it. But I guess I’m on my own there. Lol!!”

KAJA NA LULU WAKUTWA NA VIPODOZI GEREZANI



MASTAA wawili wa filamu za Kibongo walioko lupango kwa tuhuma tofauti, Kajala Masanja na Elizabeth Michael ‘Lulu’ wamedaiwa kupekuliwa na askari magereza na kukutwa na vipodozi katika Gereza la Segerea, Dar es Salaam,
Kwa mujibu wa chanzo cha ndani ya gereza hilo, mastaa hao walipekuliwa Agosti 25, mwaka huu na kukutwa na baadhi ya vipodozi ambavyo haviruhusiwi kuingizwa gerezani humo.
“Lilikuwa ni zoezi la ghafla ambalo baada ya kufanyika Lulu na Kajala walikutwa na losheni wanazozitumia,” kilisema chanzo hicho.
Chanzo hicho kilizidi kuweka bayana kuwa, mastaa hao ni warembo ambao wamezoe kila wakati kujiweka ‘sopusopu’, hivyo askari magereza walihisi watakuwa na vitu hivyo ukizingatia hivi sasa Kajala anazidi kupendeza pamoja na kwamba yupo gerezani.
“Vipodozi vile vilichukuliwa na wao kupewa onyo kwamba wasirudie kuviingiza tena gerezani la sivyo yatawapata makubwa zaidi,” kilimalizia chanzo chetu hicho.

Monday, August 27, 2012

MUIGIZAJI WA NIGERIA, TONTO DIKEH AFUNGULIWA KUPITIA EMMANUEL TV


Muigizaji wa Nollywood, Toto Diken alisema katika mahojiana kutoka na kuokolewa kwa kuacha kuvuta sigara baada ya kuomba pamoja na TB Joshua kwa kupitia Emmanuel TV. Kutokana na Tonto ambaye alianza kuvuta sigara akiwa na umri wa miaka 13, alijiunga na Nabii TB Joshua katika maombi kwa kupitia Emmanuel TV na alipokea muujiza wake katika hali ambayo hakutegemea.


Aliliambia gazeti la Burudani la Nigeria, "Nilikuwa sivuti sigara mwenyewe, Nilikuwa naangalia kipindi katika TV cha Nabii TB Joshua na alikuwa amenyoosha mikono kwa watu huku akiwaobea. Huwa napenda kuangalia vipindi vyake katika Emmanuel TV. Alipokuwa akiomba, alisema, 'Nyoosha mikono yako katika T' nikanyoosha mikono yangu siku hiyo. Hasa nilikuwa nahitaji kitu kingine kutoka kwa Mungu, na sio kuvuta sigara kwasababu napenda kuvuta! Baada ya maombi nilikaa nilipokuwa nimekaa na nikajisikia kulala usingizi. "Baada ya maombi Tonto aliamka na akajisikia kuvuta kama kawaida yake, kitu cha kujua au kugundua ni kwamba hiyo ilikuwa ni tabia yake kwa muda wa miaka 14 ya kuvuta." Nilipoamka, nilichukua sigara na nikajisikia kama nimechanganyikiwa. Sikujigundua hata kuwa nimechukua hiyo sigara kwaajili ya kuvuta. Niliona kama sumu"




One of Nollywood’s rising actresses, Tonto Dikeh, revealed in an interview that she was delivered from an addiction to smoking through praying along with Prophet T.B. Joshua on Emmanuel TV. Glory be to God!According to Tonto, who started smoking at the tender age of 13, she joined Prophet T.B. Joshua to pray on Emmanuel TV and received the miracle in a way she never expected.

She told a Nigerian entertainment magazine, “I didn’t quit smoking by myself. I was watching a program on TV with Prophet T.B. Joshua and he was laying hands on people and praying for them. I love to watch his programs on Emmanuel TV. When he was praying, he said, ‘Lay your hands on the TV’ and I just laid my hands that day. I actually needed something else from God, not to quit smoking because I loved smoking! However, after praying I sat back and I think I slept off.”After the prayer, Tonto woke up and attempted to smoke as usual, only to discover that the very habit that had been part of her for 14 years suddenly became revolting. “When I woke up, I took a stick of cigarette and I felt crazy. I couldn’t even imagine that I took it up to smoke in the first place. It felt like poison!”

Mtafsiri: Rulea Sanga (+255 715 851523)


Sunday, August 26, 2012

MSIBA WA KANUMBA VILIO UPYA

MSIBA wa aliyekuwa staa wa muvi za Kibongo, Steven Kanumba umeanza upya kwenye Kijiji cha Izigo, Muleba, Kagera baada ya mama mzazi wa marehemu, Flora Mtegoa kuupeleka msiba huo huko sanjari na mchanga wa kaburi la Dar.
Akizungumza kwa masikitiko  makubwa, mama wa Kanumba alisema tangu kifo cha mwanaye hakuwahi kupeleka msiba kijijini kwake kama mila na desturi zinavyotaka.
Aliongeza kuwa hiyo yote ilitokana na kukosa muda kwani licha ya mazishi, bado watu mbalimbali kutoka nje na ndani ya nchi walikuwa wakiendelea kumiminika nyumbani kwake kwa lengo la kumfariji.
Alisema kuwa alipofika Kagera, alipokelewa na umati wa waombolezaji na msiba ulianza upya, jambo ambalo hakulitarajia.
“Nilipofika kijijini nilipokelewa na ndugu, jamaa na marafiki, kwa kweli msiba ulianza upya. Sikutarajia, watu walilia na kuomboleza,” alisema mama Kanumba.
Akaongeza: “Kwa kweli kutokana na hali ilivyokuwa, hata mimi mwenyewe nilijikuta nalia sana. Nilihisi siku hiyo ndiyo mwanangu alifariki dunia rasmi kwa jinsi watu walivyokuwa wakiomboleza.
Akaongeza tena: “Ilibidi tufanye mambo ya mila na desturi za Wahaya zikiambatana na kuzika mchanga niliouchota kwenye kaburi la Dar (Kinondoni).
Mama Kanumba alisema anamshukuru Mungu walizika salama (mchanga) na kwamba muda si mrefu alitarajia kurejea jijini Dar kutoka kwenye msiba huo.
 “Namshukuru Mungu tumezika salama kwa kweli, mimi mwenyewe naendelea vizuri huku nikinywa dawa za Kihaya, nakaribia kurudi Dar hivi karibuni,” alisema mama Kanumba.
Steven Charles Kanumba alifariki dunia Aprili 7, mwaka huu jijini Dar es Salaam kwa madai ya kusukumwa na Elizabeth Michael ‘Lulu’ ambaye anashikiliwa na vyombo vya dola.

MFAHAMU HALIMA MDIWA(AUNT SUZY)

A.K. A: Aunty Suzy
UMRI: 25
KABILA: Mpare
KAZI YAKE: Uigizaji
MAKAZI: Kinondoni, Dar.
AMEPATAJE MAKALIO HAYO?
“Yaani ukiniuliza nimelipataje wala sina jibu kwa kuwa nimelishangaa linakuja tu tangu nikiwa mdogo. Mbaya zaidi mama yangu yuko kawaida tu, siyo mnene.”
USUMBUFU ANAOKUTANA NAO
“Umbile langu linanifanya nawakimbie wanaume, kila nikipita mara huyu kanikonyeza, mara huyu kananiita, yaani ni usumbufu mtindo mmoja.”
ANATAMANI KUPUNGUA
“Mimi natamani sana kupungua ndiyo maana natumia dawa za kupungua na kufanya mazoezi, ni kero sana.”
KUHUSU MAVAZI YAKE
“Napenda kuvaa nguo zinazonipendeza ila mara nyingi navaa zinazoficha kalio langu ili wanaume wakware wasinisumbue.”
SAIZI YA NGUO YA NDANI
“Kwa kweli sijui navaa saizi gani.”

HAPPY BIRTHDAY ODAMA

Mungu na akulinde na mabaya yote. 
Ruma Africa iko kariakoo kukutafutia mbeleko ili imsaidie mama kukubeba.

Fanya yaliyo mema siku ya leo kwani ni "Special" kwako



JAMANI LULU MATHIAS WA BONGO MOVIE, UNATUUMIZA


Aunt Lulu mbona unatuumiza kwa picha zako mitandaoni?



Saturday, August 25, 2012

FIESTA 2012: BONGO MOVIE STARS WAVAMIA MOSHI-TANZANIA



Mastaa wetu wa filamu hapa nchini, wametokelezeaje sasaaa


Wema Sepetu akijiweka sawa.


Wema Sepetu pia akizungumzia ujio wao ndani ya mji wa Moshi, kuwa wao kama Wasanii Nyota wa Filamu wamewasili mkoani humo kusaka vipaji vipya mbalimbali vya filamu, usahili huo unafanyika kwenye ukumbi wa Mr Price, ulioko mtaa wa Malindi.


Mmoja wa wasanii mahiri katika fani ya uigizaji hapa nchini, Wema Sepetu akifanya mahojiano mafupi na Millard Ayo wa Clouds FM mapema leo kwenye amsha amsha ya tamasha la Serengeti Fiesta ambalo linafanyika jioni ya leo mpaka lyamba ndani ya uwanja wa chuo cha Ushirika,ndani ya mji wa Moshi, ambapo katika tamasha hilo kiingilio kimepangwa kuwa ni nusu mnyama tu a.k.a 5,000/= kwa kila kichwa.


Msanii mwingine nyota katika tasnia ya filamu, Aunt Ezekiel akielezea ni namna tamasha la Serengeti Fiesta lilivyowambamba wakazi wa mji wa Moshi na vitongoji vyake, na pia ujio wao kuwatafuta wasanii wapya chipukizi katika tasnia hiyo ambayo imekuwa ikikua siku hadi siku.




Millard Ayo akifanya mahojiano na Ray a.k.a Vincent Kigosi kuhusiana na ujio wao ndani ya mji wa Moshi


Jacob Steven a.k.a Steven akifafanua jambo mapema leo mtaa wa Malindi kuhusiana na suala zima la wasanii hao kulivamia jiji la Moshi.



Wema na Steve Nyerere Wakiwa katika mazungumzo yao ya hapa na pale.

Kiongozi wa msafara wa tamasha la Serengeti Fiesta 2012, Mully B akiwa na mastaa wa filamu, Wema Sepetu na Aunt Ezekiel afu fulllll BBM kama kawa.


Wema Sepetu katika pozi na washabiki wake mapema mchana huu.

Pichani ni Gari aina ya Vits itakayotolewa jioni ya leo kwenye tamasha la Serengeti Fiesta 2012, kwa mshindi atakaejishindia kwenye droo itakayofanyika katika uwanja wa chuo cha ushirika, ambako tamasha hilo litarindima mpaka majogoo.

Mtangazaji wa Clouds FM,Millard Ayo akiwa Live mapema leo mtaa wa Malindi katika mpango mzima wa amsha amsha kwa wakazi wa Moshi kuhusiana na tamasha la Serengeti Fiesta 2012, ambapo pia katika tamasha hilo kutatolewa zawadi mbalimbali ikiwemo gari ndogo aina ya Vits kama uinavyo pichani ikinadiwa vilivyo.


Kawa kawa amsha amsha ya tamasha la Serengeti Fiesta pia linatoa mafuta kwa magari daladala,pikipiki sambamba na baji lita 10 ama tano kutoka kampuni ya GAPCO ambao pia ni sehemu ya wadhamini wa tamasha hilo.

Wasanii machachari Bongo Move Wema Sepetu (kushoto) na Aunt Ezekiel wakicheza muziki wa bongo Fleva uliokuwa ukishushwa na Msanii wa Bongofleva,Ferooz katika uzinduzi wa Tamasha la Serengeti Fiesta 2012 Bhaaaaass! katika Uwanja wa Chuo cha Ushirika Mjini Moshi usiku huu. Tamasha hilo limebamba ile mbaya.

Ferooz akiwa na mmoja wa mashabiki wake wakilishambulia jukwaa vilivyo.

Sehemu ya wakazi wa mji wa Moshi wakiendelea kushuhudia makamuzi ya wasanii mbalimbali wanaotumbuiza usiku huu kwenye uzinduzi wa tamasha la Serengeti Fiesta 2012.

Prezoo akiwarusha mashabiki kibao (hawapo pichani) waliojitokeza jioni ya leo kwenye uzinduzi wa tamasha la Serengeti Fiesta 2012


Pichani juu na chini ni mwanamuziki kutoka nchini Kenya na mmoja wa shiriki wa shindano la Big Brother Stargame,CMB Prezoo akitumbuiza jukwaani usiku huu kwenye uzinduzi wa tamasha la Serengeti Fiesta 2012 ndani ya uwanja wa chuo cha ushirika mjini Moshi.

Mmoja wa wasanii wa hip hop Joh Makini akikamua vilivyo usiku huu mbele ya umati mkubwa wa watu uliojitokeza kwenye uzinduzi wa tamasha la Fiesta.

Msanii mahiri wa bongofleva,Lina akiwa na densaz wake wakilishambulia jukwaa vilivyo.

Lina akiimba wimbo wake Yalaiti

Mkali mwingine wa hip hop Mwana FA akishusha mitindo huru.

Pichani juu na chini Mwana FA akilishambulia jukwaa vilivyo kwa mitindo yake huru iliyokuna vilivyo mashabiki wake,waliofika kwa wingi kwenye tamasha la Serengeti Fiesta 2012.


Wasanii wa nyota wa Filamu hapa nchini nao walijumuika kwa pamoja kwenye uzinduzi wa tamasha la Serengeti Fiesta 2012,pichani jukwaani ni Wema Sepetu,Jacob Steven a.k.a JB,pamoja na Aunt Ezekiel wakilisakata sebene.

Ray nae akilisakata sebene vilivyo.